WATU NA KAZI ZAO

  • MWANGALIZI
    mtu anayefanya kazi ya utunzaji na uhifadhi wa vitu ili visiharibike au mambo yasiende kombo
  • MWANGUZI
    mtu afanyaye kazi ya kuangusha matunda k.v-nazi kutoka mtini
  • MWANAFASIHI
    mtu anayefanya kazi ya uandishi wa sanaa ya fasihi
  • MWANAMKENDE/KISABALUU/KIBERENGE/KAHABA/MALAYA/KIBIRITINGOMA/CHANGUDOA/MTALALESHI/MLUPO/GUBERI
    mwanamke anayefanya kazi ya kujiuza au kuuza mwili wake kwa wanaume kwa ajili ya kupata pesa
  • MNDEWA/JUMBE
    mtu ambaye ni kiongozi wa jamii yake,pia huitwa balozi wa kijiji
  • MWANAMICHEZO
    mtu ambaye kazi yake ni michezo,mdau wa michezo
  • MWANAMASUMBWI/MWANANDONDI
    anayefanya kazi ya kupigana ndondi au ngumi
  • MWANAMUZIKI/MWIMBAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuimba kwa kutumia zana za muziki
  • MWANARIADHA
    anayefanya kazi ya mbio;riadha.mchezaji wa riadha
  • MWANARIWAYA
    anayefanya kazi ya kuandika vitabu vya hadithi,novela au riwaya
  • MWANASARUFU
    mtu ambaye kazi yake hushughulikia taaluma ya sarufi
  • MWANASAYANSI
    mtu ambaye kazi yake inashughulikia uchunguzi,upimaji,majaribi
  • UTEDI
    mtumishi wa cheo kidogo afanyaye kazi katika chombo cha bahari k.v kukiosha na kuwapa watu chakula
  • MAMANTILIE
    mtu hasa wa kike anayeuza chakula magengeni au nyumbani
  • MAMLUKI
    huyu ni askari wa kukodiwa ili kupigana katika nchi jirani
  • HARAMIA
    huyu ni mnyang’anyi wa baharini.Gaidi wa baharini.
  • MAKANIKA
    fundi wa kutengeneza magari au mashine
  • MANAMBA
    wafanyakazi wahamiaji katika mashamba makubwa
  • MCHINJAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuchinja wanyama na kuwauza kwenye bucha
  • MCHORAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuchora picha
  • LUGOJO
    watu wanaolinda kwa zamu
  • MFAGIZI/MFAGIAJI
    mtu anayefagia
  • MFARISHI
    mtu anayefanya kazi ya kutandika kitanda
  • MRINA
    fundi stadi wa kupakua asali
  • RUGARUGA
    mtu ambaye anafanya kazi chini ya amri ya chifu
  • KIBICHAMBO
    mtu hasa wa kike anayetumiwa kufanya kazi ya kunasa adui wa upande hasimu
  • FUNDIBOMBA
    mtu atengenezaye mifereji ya maji
  • MKWEZI
    anayepanda au kuaramia miti kv minazi na kuangua nazi
  • MFUANAZI
    mtu anayetoa makumbi kwenye nazi
  • KOSTEBO
    polisi wa cheo cha chini…


  • MNAJIMU/FALAKI/MAJUSI
    mwenye elimu na stadi wa masuala ya nyota
  • MWANDAZI
    mtu anayepika chakula kwa ajili ya shughuli za fulani k.v-sherehe,karamu nk
  • MNYAPARA/MSIMAMIZI
    mtu anayeangalia au kusimamia utekelezaji wa kazi
  • MKADIMU
    msimamizi mkuu wa shamba
  • NOKOA
    msaidizi wa mkadimu
  • MHADHIRI
    mwalimu katika chuo kikuu au chuo cha kadri anayefundisha kwa kutoa mhadhara
  • MJUME
    fundi wa kutia nakshi katika vyombo kama vile vya madini au mbao
  • TARISHI/MJUMBE/KATIKIRO/MESENJA
    mtu anayefanya kazi ya kutumwa kupeleka barua au ujumbe kutoka ofisi moja hadi nyingine au mahali mbalimbali
  • MSHENGA
    mtu anayetumwa kupeleka ujumbe au habari za kuoa-posa kutoka upande wa mchumba-mume kwa upande wa mke-mchumbiwa
  • DAKTARI/TABIBU/MGANGA
    mtu stadi katika masuala ya kuwatibu wagonjwa
  • DAKTARIMENO/MHAZIGIMENO
    huyu ni daktari wa meno
  • KULI/MPAKUZI/MPAKIZI
    mtu anayefanya kazi ya kupakua na kupakia mizigo kwenye meli,gari,bohari au mahali panapostahili
  • MSUSI/MSONZI
    anayesuka watu nywele
  • KARII
    msomaji wa Kurani


  • MWALIMU/MDARISI/USTADH
    Mtu anayefundisha
  • NAHODHA
    mtu anayeendesha meli
  • SARAHANGI
    mtu anayemsaidia nahodha(nahodha wa pili)
  • KANDAWALA
    mtu anayeendesha garimoshi
  • DEREVA
    mtu anayeendesha gari
  • RUBANI
    mtu anayeendesha ndege
  • SAISI
    mtu anayefanya kazi ya kuchunga wanyama wanaopandwa kama vile Farasi,Punda,Ngamia n.k
  • MZEGAMZEGA
    mtu anayeuza maji kwa kuyatembeza
  • MGEMA
    mtu anayefanya kazi kukinga tembo la mnazi au kuchanja magome ili kupata utomvu au kutengeneza ulimbo
  • DALALI/MNADI
    mtu anayeuza bidhaa mnadani kwa kutangaza;**Zabuni-uza kwa kushindanisha bei
  • MACHINGA/MMACHINGA
    mtu anayefanya kazi ya biashara kwa kutembeza bidhaa zake aghalabu kwa miguu ili kuwatafuta wateja mf.’Malimali’
  • MCHUKUZI/HAMALI/MPAGAZI
    mtu anayefanya kazi ya kubeba mizigo kwa kutumia rukwama,toroli,bero/baro nk
  • MCHUUZI
    mtu afanyaye kazi ya biashara ya kuuza vitu rejareja mf.Hawker!
  • MKUNGA
    mtu anayewasaidia wanawake kukopoa au kujifungua
  • NGARIBA
    mtu anayetahiri vijana jandoni au unyagoni
  • MHASIBU
    Mtu anayefanya kazi ya upimaji wa hali ya kifedha ya shirika au biashara, Mtaalamu wa kuweka hesabu za fedha. ‘Accountant
  • MHAKIKIMALI
    anayefanya kazi ya kuhakiki ubora wa bidhaa
  • MWAMIAJI/MWAMIZI
    afanyaye kazi ya kuamia ndege shamba
  • MWAMUZI
    anayesuluhisha ugomvi baina ya pande mbili au zaidi
  • REFA/MWAMUZI
    anayechezesha mchezo kulingana na sheria za mchezo husika
  • MWANAANGA
    afanyaye kazi ya utafiti wa mambo ya anga
  • MWANABAYOLOJIA
    mtaalamu wa masuala ya viumbe na mimea
  • MWANADIPLOMASIA
    mtu anayefanya kazi kv katika ubalozi
  • MWANAGAINOKOLOJIA
    mtaalamu wa maradhi ya akina mama
  • MWANAISIMU
    mtaalamu wa masuala ya isimu na lugha
  • MWANAJESHI
    askari katika jeshi la ulinzi
  • MWANAMAJI/BAHARIA/MWANAPWA
    mtu anayefanya kazi katika chombo cha baharini
  • MWANASHERIA
    mtu utaalamu wa mambo ya sheria
  • MWANASIASA
    mtu anayejishughulisha na mambo ya siasa
  • MSHAIRI/MTUNZI/MALENGA
    mtu afanyaye kazi ya kutunga mashairi/nudhuma
  • MGHANI/MANJU
    gwiji katika kuimba mashairi
  • RAWI
    stadi katika kukariri au kusoma shairi bila kuimba
  • SHAHA
    mtu stadi katika kuhariri mashairi
  • MHARIRI
    stadi katika kusoma na kukosoa kazi ilioandikwa na mtu mwengine!
  • KARII
    mtu anayesoma Kurani hasa Tajuwidi
  • KONDAKTA/TANIBOI/UTINGO/MAKANGA
    mtu anayepokea nauli kwenye gari pia hupakia na kupakua mizigo kwenye matwana,daladala au matatu
  • MSUKAJI
    mtu anayeshona,kutarizi au kufuma mkeka,jamvi,kanda au vikapu
  • BOSI/TAJIRI
    mkuu wa ofisi anayeajiri watu katika kazi
  • MRAMALI
    mtu anayetabiri mambo kwa kuvmia elimu ya nyota
  • MRATIBU
    mtu anayepanga,kuunganisha na kusimamia shughuli za watu mbalimbali katika kazi au ofisi
  • HATIBU
    mtu anayetoa hotuba kwa hadhira au hadhara
  • BAYANA
    mtu stadi au fundi wa kusema,kuongea au kuhutubu kwa kutumia ujuzi wa lugha
  • MRASIMU
    mtu anayefanya kazi ya afisi na kulingana na taratibu na kanuni za utawala
  • WADENI
    mwenye dhamana ya kusimamia mahali k.v-mbuga za wanyama,hoteli,misitu,magereza
  • WAKALA/AJENTI
    mwakilishi wa kampuni,shirika au shughuli ya kibiashara
  • WARIA
    mtu aliye hodari katika kazi za mikono mf.ushonaji,uashi,uchongaji nk
  • UTEDI
    mtumishi wa cheo kidogo afanyaye kazi katika chombo cha bahari kv-kukiosha……………..


  • MWASHI
    mtu anayejenga nyumba za mawe;anayeaka
  • SAKUBIMBI
    mtu mwenye tabia za kueneza habari za watu za uongo
  • JASUSI/MPELELEZI/NDUNZI/DUZI/MTESI
    mtu anayechunguza watu kibubusa na matukio fulani katika nchi yake au nyingine
  • KIBARAKA/KIKARAGOSI
    kiongozi wa serikali anayetumiwa ili apate mamlaka au manufaa zaidi
  • MUALISAJI/MUUGUZI/NESI
    anayehudumia wagonjwa
  • BALOZI
    kiongozi wa kidiplomasia anayewakilisha nchi yake katika nchi nyingine
  • MLANGUZI
    mtu anayenunua bidhaa kwa bei rahisi na kuviuza kwa bei ghali
  • BEPARI
    mfanyabiashara mkubwa mwenye kumiliki rasilimali au mali na njia kuu za uchumi
  • MFINYANZI
    mtu anayeunda vyombo vya udongo k.v-vyungu,kauri nk
  • DIWANI
    mtu anayewakilisha watu wake katika serikali za mitaa
  • MKALIMANI/MTARIJUMANI/MTAPTA
    anayetafsiri lugha
  • SEREMALA
    fundi anayetengeza vifa vya mbao au fanicha au samani
  • MWADHINI
    mtu anayewaita watu msikitini kwa swala
  • TOPASI/CHURA
    mtu anayefanya kazi ya usafi wa choo
  • DOBI
    anayeosha nguo au kuzipiga pasi
  • SOGORA
    stadi wa kucheza ngoma…..


  • MHASIBU
    mtu anayeweka hesabu ya fedha
  • MHAZILI/SEKRETARI
    mtu anayetunza barua na majalada ya ofisi na kuandika kwa mashine kama vile taipureta au taipu
  • MHANDISI/INJINIA
    fundi wa mitambo hasa ya vyuma
  • BAWABU/GADI/MLINZI/ASKARIGONGO/SOJA
    mtu anayelinda mali na maisha ya tajiri au bwenyenye kv viwanda,boma,shule,mashirika,ofisi nk kwa kuweka usalama
  • MKUMBIZI
    mtu anayesafisha na kuondoa takataka;pia ni mtu afuataye wavunaji shambani na kuokoteza mavuno yaliyosalia na kuuza au kutumia nyumbani
  • MSAJILI
    mtu anayeandikisha vifo,kura na kuweka orodha ya kazi au vitu alivyokabidhiwa
  • SONARA/MFUAFEDHA
    fundi wa kutengeneza mapambo k.v-pete,kekee,mkufu,bangili,kikero n.k
  • MSANA/MHUNZI/MFUACHUMA
    mtu anayefanya kazi ya kufua vitu vya madini ya chuma au bati k.v-visu,sufuria,majembe,seredani,ndusi,panga nk
  • MUKUTUBI/MKUTUBU
    mtu anayefanya kazi ya kuhifadhi vitabu na kuviazimisha kwa wasomi
  • AKIDU
    mtu anayefanya kazi kwa mkatabani
  • MUTRIBU
    mtu anayeimba nyimbo za taarabu
  • MWASHI
    anayejenga nyumba….
  • MWANASAYANSI
    mtu ambaye kazi yake inashughulikia uchunguzi,ugunduzi,upimaji,majaribio na kuthibitishwa kwa muda uliopo
  • MWANASOKA
    mtu anayefanya kazi ya kucheza mpira wa miguu,soka,kabumbu,gozi au kandanda
  • MTAALAMU
    mtu anayefanya kazi taaluma aliyotaalamika ndani yake
  • MWANATAMTHILIA/MWANATAMTHILIYA
    mtu anayefanya kazi ya kuandika michezo ya kuigiza
  • MWANAHABARI/MTANGAZAJI
    mtu anayefanya kazi ya kutafuta,kuandika,kukusanya,kuhari na kutangaza au kusambaza taarifa au habari katika vyombo vya habari
  • MWANALEKSIKOLOGRAFIA
    mtu anayefanya kazi inayoshughulikia uchunguzi,uchambuzi na uchanganuzi wa msamiati wa lugha pamoja na maana yake
  • MLEHEMAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuunganisha vitu hasa vyuma kwa kutumia madini aghalabu kwa kutumia risasi
  • MWANALEKSIKOGRAFIA
    mtu anayefanya kazi ya kuandika Kamusi
  • MSHAURINASAHA
    mtu anayefanya kazi ya kutoa ushauri au nasaha kwa watu
  • MCHANGANUZI
    mtu afanyaye kazi ya kuchanganua masuala tofautitofauti.
    Kwa hayo machache sina cha ziada.Je,una nini mdau?
  • MNAJIMU/FALAKI/MAJUSI
    mwenye elimu na stadi wa masuala ya nyota
  • MWANDAZI
    mtu anayepika chakula kwa ajili ya shughuli za fulani k.v-sherehe,karamu nk
  • MNYAPARA/MSIMAMIZI
    mtu anayeangalia au kusimamia utekelezaji wa kazi
  • MKADIMU
    msimamizi mkuu wa shamba
  • NOKOA
    msaidizi wa mkadimu
  • MHADHIRI
    mwalimu katika chuo kikuu au chuo cha kadri anayefundisha kwa kutoa mhadhara
  • MJUME
    fundi wa kutia nakshi katika vyombo kama vile vya madini au mbao
  • TARISHI/MJUMBE/KATIKIRO/MESENJA
    mtu anayefanya kazi ya kutumwa kupeleka barua au ujumbe kutoka ofisi moja hadi nyingine au mahali mbalimbali
  • MSHENGA
    mtu anayetumwa kupeleka ujumbe au habari za kuoa-posa kutoka upande wa mchumba-mume kwa upande wa mke-mchumbiwa
  • DAKTARI/TABIBU/MGANGA
    mtu stadi katika masuala ya kuwatibu wagonjwa
  • DAKTARIMENO/MHAZIGIMENO
    huyu ni daktari wa meno
  • KULI/MPAKUZI/MPAKIZI
    mtu anayefanya kazi ya kupakua na kupakia mizigo kwenye meli,gari,bohari au mahali panapostahili
  • MSUSI/MSONZI
    anayesuka watu nywele
  • MWASHI
    mtu anayejenga nyumba za mawe;anayeaka
  • SAKUBIMBI
    mtu mwenye tabia za kueneza habari za watu za uongo
  • JASUSI/MPELELEZI/NDUNZI/DUZI/MTESI
    mtu anayechunguza watu kibubusa na matukio fulani katika nchi yake au nyingine
  • KIBARAKA/KIKARAGOSI
    kiongozi wa serikali anayetumiwa ili apate mamlaka au manufaa zaidi
  • MUALISAJI/MUUGUZI/NESI
    anayehudumia wagonjwa
  • BALOZI
    kiongozi wa kidiplomasia anayewakilisha nchi yake katika nchi nyingine
  • MLANGUZI
    mtu anayenunua bidhaa kwa bei rahisi na kuviuza kwa bei ghali
  • BEPARI
    mfanyabiashara mkubwa mwenye kumiliki rasilimali au mali na njia kuu za uchumi
  • MFINYANZI
    mtu anayeunda vyombo vya udongo k.v-vyungu,kauri nk
  • DIWANI
    mtu anayewakilisha watu wake katika serikali za mitaa
  • MKALIMANI/MTARIJUMANI/MTAPTA
    anayetafsiri lugha
  • SEREMALA
    fundi au stadi anayetengeza vifa vya mbao au fanicha au samani
  • MWADHINI
    mtu anayewaita watu msikitini kwa swala
  • TOPASI/CHURA
    mtu anayefanya kazi ya usafi wa choo
  • DOBI
    anayeosha nguo au kuzipiga pasi
  • SOGORA
    stadi wa kucheza ngoma Kwa kutumia mkwiro.
  • MWANGALIZI
    mtu anayefanya kazi ya utunzaji na uhifadhi wa vitu ili visiharibike au mambo yasiende kombo
  • MWANGUZI
    mtu afanyaye kazi ya kuangusha matunda k.v-nazi kutoka kwenye mnazi
  • MWANAFASIHI
    mtu anayefanya kazi ya uandishi wa sanaa ya fasihi
  • MWANAMKENDE/KISABALUU/KIBERENGE/KAHABA/MALAYA/KIBIRITINGOMA/CHANGUDOA/MTALALESHI/MLUPO/GUBERI
    mwanamke anayefanya kazi ya kujiuza au kuuza mwili wake kwa wanaume kwa ajili ya kupata pesa
  • MNDEWA/JUMBE
    mtu ambaye ni kiongozi wa jamii yake,pia huitwa balozi wa kijiji
  • MWANAMICHEZO
    mtu ambaye kazi yake ni michezo,mdau wa michezo
  • MWANAMASUMBWI/MWANANDONDI
    anayefanya kazi ya kupigana ndondi au ngumi
  • MWANAMUZIKI/MWIMBAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuimba kwa kutumia zana za muziki
  • MWANARIADHA
    anayefanya kazi ya mbio;riadha.mchezaji wa riadha
  • MWANARIWAYA
    anayefanya kazi ya kuandika vitabu vya hadithi,novela au riwaya
  • MWANASARUFU
  • mtu ambaye kazi yake hushughulikia taaluma ya sarufi
  • MWANASAYANSI
    mtu ambaye kazi yake inashughulikia uchunguzi,upimaji,majaribi
  • UTEDI
    mtumishi wa cheo kidogo afanyaye kazi katika chombo cha bahari k.v kukiosha na kuwapa watu chakula
  • MAMANTILIE
    mtu hasa wa kike anayeuza chakula magengeni au nyumbani
  • MAMLUKI
    huyu ni askari wa kukodiwa ili kupigana katika nchi jirani
  • HARAMIA
    huyu ni mnyang’anyi wa baharini.Gaidi wa baharini.
  • MAKANIKA
    fundi wa kutengeneza magari,mashine,Injini,Meli,pikipiki au mitambo ya vyuma(Chuma)
  • MANAMBA
    wafanyakazi wahamiaji katika mashamba makubwa
  • MCHINJAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuchinja wanyama na kuwauza kwenye bucha
  • MCHORAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuchora picha
  • LUGOJO
    watu wanaolinda kwa zamu
  • MFAGIZI/MFAGIAJI
    mtu anayefagia
  • MFARISHI
    mtu anayefanya kazi ya kutandika kitanda
  • MRINA
    fundi stadi wa kuvuna na kupakua asali
  • RUGARUGA
    mtu ambaye anafanya kazi chini ya amri ya chifu
  • KIBICHAMBO
    mtu hasa wa kike anayetumiwa kufanya kazi ya kunasa adui wa upande hasimu
  • FUNDIBOMBA
    mtu atengenezaye mifereji ya maji na kuunganisha paipu za mifereji na mitaro(PLUMBER)
  • MKWEZI
    anayepanda au kuaramia miti kv minazi na kuangua nazi
  • MFUANAZI
    mtu anayetoa makumbi kwenye nazi
  • KOSTEBO
    Afisa katika kikosi Cha usalama wa Umma kama vile Polisi,Jeshi nk asiye na cheo
  • MWALIMU/MDARISI/USTADH
    Mtu anayefundisha
  • NAHODHA
    mtu anayeendesha meli
  • SARAHANGI
    mtu anayemsaidia nahodha(nahodha wa pili)
  • KANDAWALA
    mtu anayeendesha garimoshi
  • DEREVA
    mtu anayeendesha gari
  • RUBANI
    mtu anayeendesha ndege
  • SAISI
    mtu anayefanya kazi ya kuchunga wanyama wanaopandwa kama vile Farasi,Punda,Ngamia n.k
  • MZEGAMZEGA
    mtu anayeuza maji kwa kuyatembeza
  • MGEMA
    mtu anayefanya kazi kukinga tembo la mnazi au kuchanja magome ili kupata utomvu au kutengeneza ulimbo
  • DALALI/MNADI
    mtu anayeuza bidhaa mnadani kwa kutangaza;**Zabuni-uza kwa kushindanisha bei
  • MACHINGA/MMACHINGA
    mtu anayefanya kazi ya biashara kwa kutembeza bidhaa zake aghalabu kwa miguu ili kuwatafuta wateja mf.’Malimali’
  • MCHUKUZI/HAMALI/MPAGAZI
    mtu anayefanya kazi ya kubeba mizigo kwa kutumia rukwama,toroli,bero/baro nk
  • MCHUUZI
    mtu afanyaye kazi ya biashara ya kuuza vitu rejareja mf.Hawker!
  • MKUNGA
    mtu anayewasaidia wanawake kukopoa au kujifungua
  • NGARIBA
    mtu anayetahiri vijana jandoni au unyagoni
  • MHASIBU
    Mtu anayefanya kazi ya kusimamia fedha katika kampuni,shule,chuo,Benki,Kikundi au chama
  • KESHIA
    Mtu anayepokea malipo na kuandikia wanaolipa stakabadhi au risiti ya malipo
  • MWANASAYANSI
    mtu ambaye kazi yake inashughulikia uchunguzi,ugunduzi,upimaji,majaribio na kuthibitishwa kwa muda uliopo
  • MWANASOKA
    mtu anayefanya kazi ya kucheza mpira wa miguu,soka,kabumbu,gozi au kandanda
  • MTAALAMU
    mtu anayefanya kazi taaluma aliyotaalamika ndani yake
  • MWANATAMTHILIA/MWANATAMTHILIYA
    mtu anayefanya kazi ya kuandika michezo ya kuigiza
  • MWANAHABARI/MTANGAZAJI
    mtu anayefanya kazi ya kutafuta,kuandika,kukusanya,kuhari na kutangaza au kusambaza taarifa au habari katika vyombo vya habari
  • MWANALEKSIKOLOGRAFIA
    mtu anayefanya kazi inayoshughulikia uchunguzi,uchambuzi na uchanganuzi wa msamiati wa lugha pamoja na maana yake
  • MLEHEMAJI
    mtu anayefanya kazi ya kuunganisha vitu hasa vyuma kwa kutumia madini aghalabu kwa kutumia risasi(WELDER)
  • MWANALEKSIKOGRAFIA
    mtu anayefanya kazi ya kuandika Kamusi
  • MSHAURINASAHA
  • mtu anayefanya kazi ya kutoa ushauri au nasaha kwa watu
  • MCHANGANUZI
    mtu afanyaye kazi ya kuchanganua masuala tofautitofauti.
  • MSWIRIZI
    Mtaalamu wa kufuga na kucheza na wanyama hayawani kama vile Nyoka,Nyani,Sokwe nk. (SNAKE CHARMER)
  • MHAKIKIMALI
    anayefanya kazi ya kuhakiki ubora wa bidhaa
  • MWAMIAJI/MWAMIZI
    afanyaye kazi ya kuamia ndege shamba
  • MWAMUZI
    anayesuluhisha ugomvi baina ya pande mbili au zaidi
  • REFA/MWAMUZI
    anayechezesha mchezo kulingana na sheria za mchezo husika
  • MWANAANGA
    afanyaye kazi ya utafiti wa mambo ya anga
  • MWANABAYOLOJIA
    mtaalamu wa masuala ya maisha na uhai wa viumbe na mimea
  • MWANADIPLOMASIA
    mtu anayefanya kazi kv katika ubalozi
  • MWANAGAINOKOLOJIA
    mtaalamu wa maradhi ya akina mama
  • MWANAISIMU
    mtaalamu wa masuala ya isimu na lugha
  • MWANAJESHI
    askari katika jeshi la ulinzi
  • MWANAMAJI/BAHARIA/MWANAPWA
    mtu anayefanya kazi katika chombo cha baharini
  • MWANASHERIA
    mtu utaalamu wa mambo ya sheria
  • MWANASIASA
    mtu anayejishughulisha na mambo ya siasa
  • MSHAIRI/MTUNZI/MALENGA
    mtu afanyaye kazi ya kutunga mashairi/nudhuma
  • MGHANI/MANJU
    gwiji katika kuimba mashairi
  • RAWI
    stadi katika kukariri au kusoma shairi bila kuimba
  • SHAHA
    mtu stadi katika kuhariri mashairi
  • MHARIRI
    stadi katika kusoma na kukosoa kazi ilioandikwa na mtu mwengine!
  • MNUNGURI/MKONOKONO
    mganga anayewatibu walioumwa na nyoka
  • MGIMBA
    mganga anayeaminika kuwezesha mvua kunyesha au kuizuia kimuujiza
  • MGAGAJI
    mtu anayefanya biashara ya kuwauzia watu bidhaa kwa bei za juu sana kidhuluma
  • MHAZIGI/MGANGAJI
    mtu mwenye ujuzi wa kutibu viungo vya mwili vilivyovunjika. Daktari wa mifupa na nyonga za mwili.
  • MGUNDUZI
    mtu anayefanya kazi ya kugundua na kudhihirisha kitu au jambo lililokuwa limejificha au lililokuwa halijulikani
  • SHUSHUSHU
    mtu anayepeleleza maisha ya watu kwa niaba ya serikali-afisa wa usalama wa taifa(SPY)
  • KUWADI/GAWADI/KIJUMBE/GAMBERA/MTALALESHI/KIBIRIKIZI
    mtu anayepeleleza habari za siri kutoka kwa mtu fulani kuenda kwa mwengine hasa kati ya mwanamke na mwanamume
  • MSASI/MRUMBA/MWINDAJI/MKAA
    mtu anayewinda wanyama msituni akiwa na idhini
  • KIJAKAZI/MJAKAZI/KISONOKO
    mtumwa mwanamke katika nyumba;mwanamke au msichana anayefanya kazi ya nyumba
  • JANGILI
    mtu anawinda wanyama katika mbuga za wanyama bila ya idhini ya serikali
  • JEMEDARI/AMIRI
    mkuu wa majeshi
  • JAMBAZI
    mtu anayefanya kazi ya wizi Kwa kuua akitumia Silaha hatari kama vile bunduki,Bastola nk.
  • MCHOPOZI/MCHOPOAJI
    mtu anayeiba kwa kutoa mfukoni au mkobani kwa kutumia vidole viwili kisirisiri
  • MNYANG’ANYI
    mtu anayeiba kwa kunyang’anya hadharani na guvu
  • SAJINI/SAJENTI
    askari mwenye cheo kilicho daraja moja zaidi kuliko koplo
  • KOPLO
    afisa wa jeshi au polisi aliye chini ya sajini na juu ya Konstebo-Mwandamizi
  • LUTENI
    ofisa wa kijeshi aliye chini ya kapteni na juu ya luteni usu
  • KAPTENI
    ofisa wa jeshi kati ya luteni na meja
  • MEJA
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha chini yd lutenikanali na juu ya kapteni
  • MEJAJENERALI
    ofisa wa jeshi aliye juu ya brigediajenerali na chini lutenijenerali
  • BRIGEDIA
    ofisa wa kijeshi mwenye cheo cha juu ya kanali na chini ya mejajenerali
  • LUTENI-JENERALI
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha juu ya meja-jenerali na chini ya jenerali
  • LUTENIKANALI
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha juu ya meja na chini ya kanali
  • KANALI
    ofisa wa jeshi aliye juu ya lutenikanali
  • LUTENIUSU
    ofisa wa cheo cha kwanza chini ya luteni
  • OFISAUGANI/AFISAUGANI
    ofisa mwenezi wa taarifa au maarifa fulani uwandani.
  • MHAKIKIMALI
    anayefanya kazi ya kuhakiki ubora wa bidhaa Kabla havijaenda sokoni Kwa mauzo
  • MWAMIAJI/MWAMIZI
    afanyaye kazi ya kuamia ndege kwenye shamba la vyakula
  • MSHAIRI/MTUNZI/MALENGA
    mtu afanyaye kazi ya kutunga mashairi/nudhuma
  • MGHANI/MANJU
    gwiji katika kuimba mashairi
  • RAWI
    stadi katika kukariri au kusoma shairi bila kuimba
  • SHAHA
    mtu stadi katika kuhariri mashairi
  • MHARIRI
    stadi katika kusoma na kukosoa kazi ilioandikwa na mtu mwengine!
  • KARII
    mtu anayesoma Kurani hasa Tajuwidi
  • KONDAKTA/TANIBOI/UTINGO/MAKANGA
    mtu anayepokea nauli kwenye gari pia hupakia na kupakua mizigo kwenye matwana,daladala au matatu
  • MSUKAJI
    mtu anayeshona,kutarizi au kufuma mkeka,jamvi,kanda au vikapu
  • BOSI/TAJIRI
    mkuu wa ofisi anayeajiri watu katika kazi
  • MRAMALI
    mtu anayetabiri mambo kwa kuvmia elimu ya nyota
  • MRATIBU
    mtu anayepanga,kuunganisha na kusimamia shughuli za watu mbalimbali katika kazi au ofisi
  • HATIBU
    mtu anayetoa hotuba kwa hadhira au hadhara(SpeechMaker.) **Mtu anayefanya kazi ya Kuzungumza Kwa Niaba ya kampuni,shirika, Serikali,chama,Kikundi au muungano(SPOKESPERSON)
  • BAYANA
    mtu stadi au fundi wa kusema,kuongea au kuhutubu kwa kutumia ujuzi wa lugha
  • MRASIMU
    mtu anayefanya kazi ya afisi na kulingana na taratibu na kanuni za utawala
  • WADENI
    Afisa mwenye dhamana ya kusimamia mahali k.v-mbuga za wanyama,hoteli,misitu,magereza(WARDEN/GAMEPAEK RANGER)
  • WAKALA/AJENTI
    mwakilishi wa kampuni,shirika au shughuli ya kibiashara
  • WARIA
    mtu aliye hodari katika kazi za mikono mf.ushonaji,uashi,uchongaji nk(ARTISAN)
  • UTEDI
    mtumishi wa cheo kidogo afanyaye kazi katika chombo cha bahari.
  • GADI/BAWABU/MLINZI/ASKARIGONGO
    Afisa wa usalama wa kibinafai anayefanya kazi ya Kulinda Uhai na Mali ya tajiri.
  • HADIMU
    Mtu anayefanya kazi ya kuwahhdumia wateja katika hoteli,mkahawa,mgahawa,dukani,supamaketi nk(WAITER)
  • NESI
    Mhudumu Afya anayewashughulikia wagonjwa katika hospitali au nyumbani.
  • MCHOPOZI/MCHOPOAJI
    mtu anayeiba kwa kutoa mfukoni au mkobani kwa kutumia vidole viwili kisirisiri
  • MNYANG’ANYI
    mtu anayeiba kwa kunyang’anya hadharani na guvu
  • SAJINI
    askari mwenye cheo kilicho daraja moja zaidi kuliko koplo
  • KOPLO
    afisa wa jeshi au polisi aliye chini ya sajini
  • LUTENI
    ofisa wa kijeshi aliye chini ya kapteni na juu ya luteni usu
  • KAPTENI
    ofisa wa jeshi kati ya luteni na meja
  • MEJA
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha chini yd lutenikanali na juu ya kapteni
  • MEJAJENERALI
    ofisa wa jeshi aliye juu ya brigediajenerali na chini lutenijenerali
  • BRIGEDIA
    ofisa wa kijeshi mwenye cheo cha juu ya kanali na chini ya mejajenerali
  • LUTENI-JENERALI
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha juu ya meja-jenerali na chini ya jenerali
  • LUTENIKANALI
    ofisa wa jeshi mwenye cheo cha juu ya meja na chini ya kanali
  • KANALI
    ofisa wa jeshi aliye juu ya lutenikanali
  • LUTENIUSU
    ofisa wa cheo cha kwanza chini ya luteni
  • OFISAUGANI/AFISAUGANI
    ofisa mwenezi wa taarifa au maarifa fulani uwandani


Print Friendly, PDF & Email
Tell your friends about this content:



Leave a Reply 0